Nenda kwa yaliyomo

Joshua Mutale

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Joshua Mutale (alizaliwa Lusaka, Zambia, 24 Januari 2002) ni mchezaji wa mpira wa miguu.

Alianza safari yake ya soka akiwa na Power Dynamos, klabu ya Zambia, ambapo alijiunga mnamo Oktoba 2020. Katika klabu ya Power Dynamos, Mutale ameonyesha uwezo wake kama kiungo wa kati na aliweza kucheza michezo mingi na kufunga mabao muhimu[1]

Mutale pia ni mchezaji wa timu ya taifa ya Zambia, ambapo amecheza michezo kadhaa tangu alipofanya debut yake mnamo Machi 2022. Ameonyesha uwezo mkubwa katika timu ya taifa, ingawa bado hajaweza kufunga bao lolote kwa timu hiyo.

Mnamo Julai 2024, Mutale alihamia Simba S.C., klabu ya Tanzania, na kusaini mkataba wa miaka mitatu utakaomalizika Julai mwaka 2027. Hii ni hatua kubwa katika taaluma yake, kwani Simba S.C. ni mojawapo ya klabu yenye mafanikio Afrika Mashariki[2].

Makala hii kuhusu mchezaji mpira fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Joshua Mutale kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.